×

Używamy ciasteczek, aby ulepszyć LingQ. Odwiedzając stronę wyrażasz zgodę na nasze polityka Cookie.


image

Habari za UN, Kambini Za’atari, mkimbizi kutoka Syria ageuza takataka kuwa hazina nchini Jordan | | Habari za UN

Kambini Za'atari, mkimbizi kutoka Syria ageuza takataka kuwa hazina nchini Jordan | | Habari za UN

Katika kambi ya wakimbizi ya Za'atari iliyoko nchini Jordan, roho ya ubunifu ya mtu mmoja na dhamira yake isiyoyumba imebadilisha vitu mbalimbali vinavyotupwa na kuonekana havifai tena kuwa nyenzo muhimu za urembo.

Ziyad Al-Awaji, al maarufu Abu Jihad, kila siku huamka alfajiri kuaza shughuli zake za kutafuta plastiki iliyotupwa na vifaa vingine kwenye dampo za taka katika kambi ya wakimbizi ya Za'atari huko nchini Jordan.

Mkimbizi huyu kutoka nchini Syria mwenye umri wa miaka 64, mume na baba wa watoto 12 pamoja na kupitia magumu ikiwa ni pamoja na kupoteza nyumba yake na kipato sababu ya vita nchini mwake, hajakata tamaa na amedhamiria kuleta athari chanya kwa jamii yake na mazingira.

Tangu awasili kambini hapo mwaka 2013 Abu Jahid alianza kujenga nyumba yake na kuiremba na vitu vya kipekee kutoka majalalani. Mapenzi yake ya kuchakata malighafi zilizotupwa yalichochewa na rasilimali chache zinazopatikana kambini, na punde si punde akawa gwiji wa kutafuta matumizi mapya ya vitu vya zamani na kugeuza taka anazo okota kuwa vitu muhimu na vizuri.

"Hii ni Chandelier, lakini bado haijakamilika, hii hapa ni mashine ya kusagia kahawa. "Ninatumia tena nyenzo zozote zinazokuja mikononi mwangu. Ninapenda kutoa maisha ya pili kwa vitu ambavyo tunadhani ni upotevu. Kila kitu kina matumizi ya pili,”

Mbali na ubunifu wake wa kutengeneza vitu kama meza, taa, matanki ya kuhifadhi maji ya mvua na mifuko lakini Abu Jahid ni mfano mzuri wa namna wakimbizi wanaweza kuwa na athari chanja katika jamii zao.

“Jordan inatuchukulia kama raia wake, tumekumbatiwa na kuungwa mkono kwa namna ambazo zinatufanya tujisikie kama sehemu ya jamii ya Jordan.”

Wakati dunia inapambana na athari mbaya za uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na plastiki, shauku ya Abu Jihad ya kuchakata tena taka ni mfano mzuri wa namna uwezo na vitendo vya mtu binafsi unavyoletwa kuleta mabadiliko katika dunia.

Kambini Za'atari, mkimbizi kutoka Syria ageuza takataka kuwa hazina nchini Jordan | | Habari za UN Im Lager Za'atari verwandelt ein Flüchtling aus Syrien in Jordanien Müll in Schätze | UN-Nachrichten In Za'atari camp, a refugee from Syria turns trash into treasure in Jordan | UN news En el campo de Za'atari, un refugiado de Siria convierte la basura en un tesoro en Jordania | noticias de la ONU Dans le camp de Zaatari, un réfugié syrien transforme ses déchets en trésor en Jordanie | Actualités de l'ONU ザータリキャンプでシリアからの難民がヨルダンでゴミを宝物に変える|国連ニュース No campo de Za'atari, um refugiado da Síria transforma lixo em tesouro na Jordânia | notícias da ONU

Katika kambi ya wakimbizi ya Za'atari iliyoko nchini Jordan, roho ya ubunifu ya mtu mmoja na dhamira yake isiyoyumba imebadilisha vitu mbalimbali vinavyotupwa na kuonekana havifai tena kuwa nyenzo muhimu za urembo.

Ziyad Al-Awaji, al maarufu Abu Jihad, kila siku huamka alfajiri kuaza shughuli zake za kutafuta plastiki iliyotupwa na vifaa vingine kwenye dampo za taka katika kambi ya wakimbizi ya Za'atari huko nchini Jordan.

Mkimbizi huyu kutoka nchini Syria mwenye umri wa miaka 64, mume na baba wa watoto 12 pamoja na kupitia magumu ikiwa ni pamoja na kupoteza nyumba yake na kipato sababu ya vita nchini mwake, hajakata tamaa na amedhamiria kuleta athari chanya kwa jamii yake na mazingira.

Tangu awasili kambini hapo mwaka 2013 Abu Jahid alianza kujenga nyumba yake na kuiremba na vitu vya kipekee kutoka majalalani. Mapenzi yake ya kuchakata malighafi zilizotupwa yalichochewa na rasilimali chache zinazopatikana kambini, na punde si punde akawa gwiji wa kutafuta matumizi mapya ya vitu vya zamani na kugeuza taka anazo okota kuwa vitu muhimu na vizuri.

"Hii ni Chandelier, lakini bado haijakamilika, hii hapa ni mashine ya kusagia kahawa. "This is a chandelier, but it's not finished yet, here's a coffee grinder. "Ninatumia tena nyenzo zozote zinazokuja mikononi mwangu. Ninapenda kutoa maisha ya pili kwa vitu ambavyo tunadhani ni upotevu. Kila kitu kina matumizi ya pili,”

Mbali na ubunifu wake wa kutengeneza vitu kama meza, taa, matanki ya kuhifadhi maji ya mvua na mifuko lakini Abu Jahid ni mfano mzuri wa namna wakimbizi wanaweza kuwa na athari chanja katika jamii zao.

“Jordan inatuchukulia kama raia wake, tumekumbatiwa na kuungwa mkono kwa namna ambazo zinatufanya tujisikie kama sehemu ya jamii ya Jordan.”

Wakati dunia inapambana na athari mbaya za uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na plastiki, shauku ya Abu Jihad ya kuchakata tena taka ni mfano mzuri wa namna uwezo na vitendo vya mtu binafsi unavyoletwa kuleta mabadiliko katika dunia.